WAGANGA WA TIBA ASILI WANOLEWA ILI KUWAONGEZEA MAARIFA.
Na Mwandishi wetu Mwanza
Waganga wa tiba asili na tiba mbadala mkoa wa Mwanza wamepatiwa elimu mahususi yenyekuwajengea uwezo na maarifa katika utendaji kazi wa utoaji huduma ya tiba kwa wananchi.
Akitoa elimu hiyo kwa waganga wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza katibu mkuu wa chama cha waganga wa tiba asili na tiba mbadala Bw Lukas Joseph Mlipu amesema kwamba chama hicho kimejenga misingi mbalimbali ikiwemo ya kuwapa elimu waganga wanaojiunga na chama hicho kwa lengo la kuchechemua taaluma hiyo ambayo imekuwa ikizipitia changamoto nyingi kutokana na sababu tofauti tofauti ikiwemo ya waganga kuchukuliwa kama watu wasiokuwa na elimu jamba ambalo siyo sahihi hivyo ili kuiondoa dhana hiyo kwa jamii TAMESOT iliona vyema kuanzisha mpango mahususi wa kuwasadia waganga kwa kuwapa elimu wanaojiunga na chama hicho.
Bw Mlipu akiwa darasani amesema ili kuyafanikisha malengo hayo tayari kwa umahiri mkubwa chama kimechapisha vitabu kadhaa ambavyo ndani yake vipo vya miongozo kwa viongozi na miongozo ya wanachama sambamba na vitabu vya katiba na kanuni za TAMESOT.
Kiongozi huyo pia amesema yuko kwenye ziara ya mikoa 10 akiendelea kukutana na waganga pamoja na wadau likiwemo jeshi la polisi akiendelea kuwahamasisha mambo muhimu likiwemo suala la kupata uongozi imara kuanzia ngazi ya kitaifa hadi ngazi ya chini ili kushirikiana na mamlaka za serikali katika kuwaunganisha pamoja waganga hatimaye waweze kufanya kazi zao kwa uhuru bila kubughudhiwa.
Amafafanua kuwa tayari ziara yake imeifikia mikoa minne ya Mbeya, Shinyanga, Geita , Mwanza na bado anaendelea na mikoa mingine ukiwemo mkoa wa Mara.
Akiwa mkoa ni Mwanza katibu mkuu Lukas hakusita kukemea watu wanaotumia mwavuli wa tiba asili kinyume na taratibu ili kushiriki ramli chonganishi kwa jamii jambo ambalo amesema halivumiki huku akisisitiza kuwa TAMESOT itaendelea kuwakemea watu wanamna hiyo kwani hawana nia njema na taba asili badala yake wamekuwa ni watu wenye kuichafua kwa matukio maovu ikiwemo ya kuwaibia wananchi na hayuko tayari kumuona mwanachama wa TAMESOT akishiriki ramli chonganishi.
Ametoa wito kwa waganga wa tiba asili na tiba mbadala kushikamana na kuwa wamoja katika majukumu ya kuwasadia tiba wananchi tena kwa ufanisi ambapo amewahimiza kuhakikisha wanashiriki matukio yanayowakusanya kwa pamoja likiwemo tukio linalotarajia kuwakutanisha hivi karbuni waganga na waziri wa afya mkoani Dodoma.
Nao waganga wa mkoa huo wa Mwanza wamepongeza na kushukuru ujio wa ziara ya katibu mkuu Lukas kutokana na alivyowapatia elimu na maarifa kadha wa kadha nakuwaongezea mwanga zaidi katika majukumu yao ya kutoa tiba hivyo nao hawakusita kuwakemea watu wanaoshiriki ramli chonganishi wakisema kuwa kutokana na madhara ya ramli hiyo watu wanamna hiyo hawanabudi kushughulikiwa ili kuyakomesha matukio yakikatiri ambayo mara kadhaa yamekuwa yakijiri kwa jamii.
.jpeg)
