ZITTO KABWE AGUSWA NA KILIO CHA WAFANYABIASHARA WA SAMAKI MWANZA, ATOA RAI KWA RAIS MAGUFULI.

 
Mbunge wa Kigoma mjini ambaye pia ni kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO Mhe. Zitto Kabwe, asubuhi ya leo Januari 28, 2018 ameonyesha kuguswa na kilio cha wafanyabiashara wa samaki jijini Mwanza.
Akiandika kwenye ukurasa wake wa Twitter Zitto amemkumbusha Mhe. Rais Magufuli kuhusu adha ya uliopaji kodi wanayokumbana nayo wafanyabiashara hao kwa samaki wanaosafirishwa kwenda kwenye mikoa ya mpakani mwa nchi kutoa mwaloni Kirumba jijini Mwanza.
Mhe. Zitto amenukuu kichwa cha habari cha gazeti moja la mtandaoni na kisha kuwatag Mheshimiwa Rais Magufuli na viongozi wengine, pamoja na vyombo kadhaa vya habari ili kufikisha ujumbe wake huo.
RAIS MAGUFULI TUSAIDIE: WAFANYABIASHARA WA SAMAKI MWANZA WALIA ametweet Zitto akinukuu moja ya gazeti hapa nchini.
Wafanyabiashara wa samaki katika soko la mwaloni Kirumba jijini Mwanza, kwa siku za hivi karibuni wamekuwa wakilalamikia utaratibu mpya wa kulipia kodi samaki ambao wamekuwa wakisafirishwa kwenda kwenye baadhi ya mikoa ambayo ipo mpakani mwa nchi.
Utaratibu huo mpya umeonekana kuwaathiri sana wafanyabiashara hao jambo lililopelekea kutokea kwa migomo ya mara kwa mara ikiwahusisha wafanyabiashara hao kushinikiza kuondolewa kwa utaratibu mpya huo ambao unaonekana kuwanyonya.
Wafanyabiashara hao ambao idadi yao ni zaidi ya 2000, wamemuomba Mhe. Rais Magufuli kusikia kilio chao hicho na kutatua mgogoro ambao umekuwepo kwa muda sasa kati ya Ofisi ya Mkoa wa Mwanza, wawakilishi wa wizara ya Uvuvi na Mifugo, pamoja na mamlaka ya mapato nchini yaani TRA.
Powered by Blogger.