KUELEKEA UCHAGUZI WA MARUDIO SIHA, CHADEMA WAPATA PIGO ZITO



Kilimanjaro. Mchana wa leo Jumapili Januari 28, 2018, taarifa za kuaminika kutoka katika kata ya Ormelili wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro zinasema chama cha CHADEMA kimekimbiwa na viongozi wake.
Viongozi wanaodaiwa kukimbia ni kutoka kata ya Ormelili ambao kwa pamoja wamejiuzulu nafasi zao na kujivua uanachama wa chama hicho, hivyo kuomba kujiunga na chama cha CCM.
Taarifa zaidi zinasema na aliyekuwa mfadhili wa ofisi za chama katika kata hiyo Bi. Janneth Mamboleo Mushi nae amekikacha chama hicho na kujiunga na CCM ambapo pia amechukua nyumba yake na kuwafanya CHADEMA kukosa ofisi katika kata hiyo.
Viongozi hao wamepokelewa na ndugu Humprey Polepole ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa, alipokuwa kwenye kampeni za kumnadi mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Siha.
Hili ni pigo lingine zito kabisa kwa CHADEMA ambapo ni masaa machache tu yamepita toka walikuwa madiwani wa viti maalumu kupitia chama hicho kujiuzulu na kujiunga na CCM huko wilayani Rombo.
 SOURCE DARMPYA.
Powered by Blogger.