SIMIYU;MAPYA YAIBUKA WENYE VYETI FEKI.

 
 
 
 
.Waanza kuyakimbia madeni waliyokopa,
.Wategemezi wao wahaha kukosa wasaidizi.
 
SIKU chache baada ya serikali kutangaza na kuyaweka hadharani majina ya watumishi wa Umma wenye vyeti feki baadhi yao wameanza kuyakimbia madeni walikopa kwa watu binafsi, huku wategemezi wao wakikosa mahali pa kukimbilia.

Kufuatia uchunguzi uliofanywa na waandishi wa Habari mkoani Simiyu umebaini kuwa baadhi ya watumishi wa umma hasa walimu waliokuwa wamekopa kwa watu binafsi waeanza kukimbilia kusikojulikana huku baadhi yao wakizima simu na kuyahama makazi yao kimyakimya.

Mashaka Magembe mmoja wa wafanyabiashara mjini Bariadi alisema kuwa amekuwa akiwakopesha walimu kwa riba, lakini baada ya kubaini kuwa baadhi yao wameondolewa katika utumishi wa umma kwa kuwa na vyeti feki alianza kuwatafuta ili kulipa madeni lakini hakufanikiwa.

‘’baada ya kuyaona majina yao katika orodha ya watumishi hewa, niliwapigia simu lakini hawakuweza kunipa ushirikiano kama awali…mmoja nilikuwa namdai laki tatu, nilipompigia simu alisema tukutane mtaani badala ya nyumbani kwake na nilipofuatilia kwake nikakuta ameshahama’’ alisema Magembe.

Aliongeza kuwa baadhi yao wamerejesha fedha kidogo huku wakisema kuwa hali imekuwa mbaya kulingana na majina yao kubainika katika orodha ya watumishi huku wakiahidi kuwasimamishia riba na watakuwa wanalipa kidogokidogo.

Alisema kuwa Mwalimu mmoja (jina linahifadhiwa) hadi sasa hajui aliko na simu yake wakati huo ameshahama alipokuwa anaishi ambapo kwenye mkataba wa mkopo aliweka dhamana ya seti ya kochi, tv, friji na kitanda.
Kwa Joel Peter ambaye ni Mwanafunzi wa chuo cha Ualimu Tabora alisema kuwa kwa sasa hataweza kumalizia masomo yake kutokana na wategemezi wake wote kubainika wana vyeti  feki.

Alisema kuwa kaka yake ambaye ni Mwalimu huko Itilima amebainika ana vyeti feki hivyo amekuwa na wasiwasi juu ya upatikanaji wa fedha za kumalizia masomo yake ya ualimu.

‘’Japhet Lasphord Katembo na mke wake wote wamebainika na vyeti feki na ndiyo walikuwa wakinisomesha, sasa sijui itakuwaje na wazazi wangu walishafariki’’ alisema Joel huku akiiomba serikali kunagalia namna ya kuwasaidia wanafunzi walioko masomoni.

Aidha kufuatia agizo la Rais Magufuli la kuwataka watumishi wenye vyeti feki kutoonekana maofisini baadhi ya maafisa utumishi mkoani Simiyu wameanza kuwatumia barua za kufukuzwa kazi kwa watumishi hao mara moja.
 
Na mwandishi wa MAKALIBLOG;  COSTANTINE MTAHIAS, SIMIYU.

Powered by Blogger.