GRUMETI FUND WASHEREHEKEA SIKU YA TWIGA DUNIANI.
Watanzania wametakiwa kuendelea kumlinda na
kumthamini twiga, ambaye ni nembo ya Taifa la Tanzania, kwa kutambua mchango
wake katika kutangaza utalii, kuhifadhi urithi wa asili na kuwajengea watoto na
vijana uelewa kuhusu umuhimu wa Twiga na kudumisha utambulisho wa Taifa .
Kila ifikapo juni 21 dunia huadhimisha siku ya
Twiga na kwa Tanzania Mnyama huyu hutumika kama nembo ya Taifa wadau wa
uhifadhi Grumeti Fund kupitia idara ya Utafiti na Ubunifu wameanzisha program ya
elimu ya Uhifadhi kwa wanafunzi wa shule za msingi ikiwa juhudi za kuendeleza
uhifadhi wa wamnyama huyo kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa
idara Utafiti na Ubunifu Grumeti Fund Dk.George Lohay alisema wameanza kujenga
elimu hiyo kwa watoto ilikuwasaidia kuutambua uhifadhi kwa watoto wakiwa wadogo nahiyo nikutimiza lengo la kuwarithisha.
“Tunamsherehekea Mnyama Twiga ninembo Taifa
nimnyama Mpole ambae pia anapendwa sana na watalii kwahiyo watoto walioko
katika hifadhi tunajitahidi sana kuwafundisha watoto”Alisema Dkt George Lohay
Mkuu wa Idara Rise Grumeti Fund.
Kwa uapnde wake mkuu kitengo cha maliasili na
ufadhi wa mazingira wilaya ya Bunda Marwa Kitende alisema asilimia kubwa wilaya
ya Serengeti inazungukwa na mapori mengi hivyo kuwafundisha watoto itasaidia
kuwapa ulewa watoto waweze kuulewa Uhifadhi.
Aidha naye Afisa uhusiano Ujirani mwema Ikorongo na Grumeti Shija Alex amesema kwa sasa mahusino ya imarika kutoka katika kijiji vinavyoishi katika Mapori hayo ya ikorongo na Grumeti wamekuwa na ulewa mzuri dhidi ya Uhifadhi kutokana na elimu inayotolewa mara kwa mara huku wananchi wakiomba matamasha hayo kuendelea mara kwa mara ilikuendelea kujenga Elimu ya ulelewa kwa wananchi.