MARA-RC WAHISI UJANJA UJANJA BODI YA PAMBA WASHINDWA KUTEKELEZA MAAGIZO YA MKUTANO MKUU;
MAKALIBLOG; SIMIYU;
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Dkt.Rehema Nchimbi (wa pili kushoto) akichangia jambo wakati wa ziara ya wakuu wa mikoa ya Kanda ya Magharibi inayolima pamba walipotembelea mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora ya pamba(UKM08) katika kata ya Mwabusalu wilayani Meatu(kulia) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mhe.Festo Kiswaga ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Dkt.Rehema Nchimbi (wa pili kushoto) akichangia jambo wakati wa ziara ya wakuu wa mikoa ya Kanda ya Magharibi inayolima pamba walipotembelea mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora ya pamba(UKM08) katika kata ya Mwabusalu wilayani Meatu(kulia) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mhe.Festo Kiswaga ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka.
Wakati lawama kubwa za wakulima wa pamba zikiwa ni
kuuziwa mbegu zisizoota na dawa zisizokuwa na ubora, wakuu wa mikoa inayolima
zao hilo wasema bodi ya pamba Tanzania (TCB) inaendeshwa kiujanja ujanja.
Wakuu hao wa mikoa inayolima
zao la pamba nchini wamesema kuwa bodi ya pamba wameshindwa kutekeleza maagizo
ya mkutano mkuu wa wadau wa kuwa na mashamba ambayo yatakuwa yakitumika kwa
ajili ya kuzalisha mbegu za zao hilo.
Hayo yalibainishwa juzi na wakuu wa
mikoa hiyo yaShinyanga,Geita,Singida, Kigoma ,Tabora na Simiyu wakati wa ziara
ya kutembelea shamba la mfano lililopo katika kijiji cha Mwabusalu Wilayani
Meatu walipokwenda kujifunza jinsi ya kulima zao hilo ikiwemo mbegu ya Ukm 08.
Akiongea kwenye Shamba hilo Mkuu wa
mkoa wa Geita Meja Jenerali mtaafu Ezekiel Kiunga alisema kuwa bodi ya pamba
wamekuwa wajanjawajanja na wameshindwa kutekeleza maagizo waliyopewa ya kuwa na
mashamba yao wenyewe ya kuzalisha mbegu na badala yake wanatumia mashamba ya
wananchi.
“Bodi ya pamba inaendeshwa kihuni
kila wakipewa maelekezo wanashindwa kutekeleza kutekeza mwaka jana katika
mkutano mkuu tuliwataka kuanzisha mashamba yao ya kuzalisha mbengu ya pamba ili
kuondokana na kutegemea kutoka kwa wananchi lakini bado wanategemea wananchi
kuzalisha”alisema Kiunga.
Alibainisha kuwa wanakuwa na
wasiwasi na utendaji kazi wa bodi ya pamba kwani yale wanayokubaliana kwenye
vikao yanabaki kwenye makaratasi na kushindwa kufanyiwa kazi na kubaki
kuwaumiza wananchi wanaolima zao hilo.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa
Tabora Agrey Mwanri alisema kuwa kilimo cha pamba kitakufa endapo
wananchi hawatawezeshwa kuingia katika kilimo cha mkataba ambacho
ataingia na mnunuzi moja kwa moja kwani itawawezdesha kupata mahitaji yote ya
pembjeo.
“njia pekee ya kumsaidia mwananchi
anaylima zao hili ni kumuweka katika kilimo cha mkataba kwani ataweza kupata
pembejeo kwa bei nafuu kulimo kumwacha anajigharamia mwnyewe kwani inafika
mahali mkulima huyu anakosa hela ya kuhudumia”alisema Mwanri.
Naye Mkuu wa mkoa wa Singida Dk
Rehema Nchimbi alisema ni bora bodi iwe inafanya tafiti katika maeneo
mbalimbali ya mbegu za pamba kwani eneo la simiyu halifanani na eneo la mkoa wa
singida hivyo mbegu zinazostawi simiyu singida haziwezi kustawi ni bora
ikaangaliwa njia nyingine za kuzifanyia mazoezi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni
ya kuchambua pamba la Gaki kutoka shinyanga Gasper Kileo alisema kuwa njia
peke ya kuweza kuingia katika kilimo cha mkataba ni kuazisha ushirika na
kufufua iliyokuwa mifuko ya ushirika ambao watakuwa wanasimamiwa na serikali
wataweza kufanya kazi vizuri na wakulima.
Alibainisha kuwa lazima ushirika
wafanye uchaguzi na usimamiwe na serikali kwani tukiwaacha wenyewe hawataweza
kupata viongozi ambao wataweza kuwasaidia wananchi na kutatua changamoto zao.
Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba, Marco Mtunga akitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali kwa wakuu wa mikoa ya Kanda ya Magharibi inayolima pamba walipotembelea mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora ya pamba(UKM08) katika kata ya Mwabusalu wilayani Meatu
Baadhi ya Wakuu wa mkoa ya Kanda ya Magharibi inayolima pamba wakati wa ziara yao walipotembelea mashamba ya uzalishaji wa mbegu bora ya pamba(UKM08) ya katika kata ya Mwabusalu wilayani Meatu.
KWA USHAURI UNAWEZA KUTUPIGIA KUPITIA
0754295996,0789524987 ‘’’ MATUSI HAPANA