MGANGA HOSPITALI, MBARONI KWA KUOMBA RUSHWA YA SHILINGI Tshs.20000 KWA MJAMZITO;



 
 Na.MAKALIBLOG.MARA.
Tasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Mkoani mara imemfikisha mahakamani mganga wa hospitali ya wilaya Tarime Samweli Isaya obierokwa kosa la kudai na kupokea rushwa kiasi cha shilingi elf ishirini 20000/= ,
kutoka kwa magesa kihongo ili aweze kumhudumia mkewe aliekuwa mjamzito.

Obiero akiwa mwajiriwa wa halmashauri ya tarime katika hospitali hiyo alipokea kiasi hicho cha fedha kutoka kwa mwananchi ambae alifika na mkewe kwa ajiri ya kupata matibabu kutokana na na tatizo la ujauzito lilokuwa likimkabili.

Kwa kutambua kuwa hilo nikosa kisheria lakini tabibu huyo anadaiwa kuomba kiasi hicho cha fedha ilihali yeye akiwa ni mtumishi wa umma anaestahili kutoa huduma hiyo,

Wakati huo huo tasisi hiyo pia imempandisha kizimbani mkuu wa soko la Bweri Maanya manyama kwa kosa la kupokea rushwa kiasi cha shilingi elf kumi nambili kutoka kwa mtu mmoja ambae jina lake limehifadhiwa baada ya kukutwa akijisaidia katika maeneo yasiyo ruhusiwa ndani ya soko hilo.

Ambapo inadaiwa kuwa maanya akiwa mkuu wa soko hilo akishirikiana na askari mgambo Wiliam mafuru walipokea kiasi hicho cha pesa ili wasimchukulie hatua za kisheria mwananchi aliekutwa akijisaidia katika eneo hilo lisilo ruhusiwa.

Kwa kutambua kuwa kitendo cha kupokea rushwa nikinyume cha sheria kifungo cha 15(1) (a) yakuzuia na kupambana na rushwa  ya mwaka 11/2017.

 maanya manayama alikana  mashitaka yake na kutakiwa kuwa na wadhamini wawili kwa dhamana ya maandishi ya million nne kila mmoja hivyo akashindwa kutimiza masharti hayo na kupelekwa mahabusu.

Mahakama imetoa hati ya kupelekwa kwa washitakiwa Wiliam Mafuru na Victor  Chrisma,ambapo washitakiwa hao wawili wapo mahabusu katika kesi nyingine namba CC37/2017.

Aidha kesi hiyo ya rushwa namba CC 299/2017 imefikishwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Mwinyi yahaya  na iko mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo Mheshimiwa Amon Kahimba.
Powered by Blogger.