NAKULETEA KARIBU YAKO ZIARA YA GRACA MACHEL MKOANI MARA LENGO NIKUHIMIZA ELIMU:MATUKIO NA PICHA UTAYAPATA ANGALIA

GRACA MACHEL ASISITIZA SUALA LA ELIMU MKOA WA MARA AFANYA ZIARA BUTIAMA ANGALIA MATUKIO KATIKA PICHA

Mama Graca Machel aliyekuwa mke wa Rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela akiongea na wanafunzi wa Shule ya Msingi Nyamisisi Wilayani Butiama Mkoani  Mara wakiwemo wanafunzi wa MEMKWA. baada ya kuzindua mradi wa kuwapatia elimu wanafunzi 20,000 katika mfumo wa nje ya shule kutoka Wilaya ya Tarime, bunda, Butiama, na Musoma.

Wakwanza kutoka kushoto ni Meneja Mradi kutoka Mara Alliance Godfrey Wawa akifuatiwa na Mwanzislishi wa MEMKWA  Naomi Katunzi na wa pili kutoka kulia ni Graca  Machel na wakwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Butiama Annarose Nyamubi.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Butiama wakitoa Burudani mbele ya mgerni rasmi



Wanafunzi ambao wako nje ya mfumo wa shule MEMKWA katika shule ya msingi Nyamisisi wakisikilia Graca Machel baada ya kutembelea shule hiyo

Wanafunzi ambao wako nje ya mfumo wa shule MEMKWA katika shule ya msingi Nyamisisi wakisikilia Graca Machel baada ya kutembelea shule hiyo

Akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Butiama

Mkuu wa wilaya ya Butiama Annarose Nyamubi akicheza ngoma

Graca Machel akicheza ngoma na wanafunzi wa shule ya msingi Nyamisisi


Mkuu wa wilaya ya Butiama akiongea na wanafunzi pamoja na wazazi ambapo amesisitiza suala la Elimu kwa watoto wote huku wazazi na walezi wakiondokana na suala zima la kuozesha watoto wa kike katika umri mdogo.



Kulia ni Mwanzilishi wa MEMKWA Tanzania Naomi Katunzi akisisitiza umhimu wa Elimu ya MEMKWA

Mkuu wa wilaya ya Butiama Annarose Nyamubi akikumbatia Graca Machel kwa Furaha




Graca Machel akiongea na wanafunzi wa shule ya msingi Nyamisisi Butiama  na kusistiza suala zima la umhimu wa Elimu.



Graca Machel akiongea na wazazi walezi wa wanafunzi  wakiwemo wanafunzi wa MEMKWA amesema kuwa wazazi watoe yushirikiano wa kutosha ili kuwezesha watoto wao kutimiza ndoto ya kielimu.



Wanafunzi wa MEMKWA wakiwa shuleni japokuwa bado wanakumbwa na changamoto ua ukosefu wa vyumba vya madarasa madarasa siyo rafiki kwa elimu wanayoipata Mvua ikinyesha ni changamoto pamoja na jua kwani majengo yanayotumika bado hayajaezekwa katika shule ya Msingi Nyamisisi Wilayani Butiama Mkoani Mara.


Graca Machel akiwa darasani

Wanafunzi wa MEMKWA katika picha ya pamoja


Graca Machel akipanda Mti kwa ajili ya kumbukumbu katika shule ya msingi Nyamisisi Butiama

Powered by Blogger.