WATOTO WANNE WAJERUHIWA KWA MOTO NYUMBA ZAFIKA 12 ZILIZOUNGUA NYAMONGO, MBUNGE ATOA MSAADA WA GODORO NA CHAKULA.


PICHA YA MWITA CHACHA AKIWA AMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA NYANGOTO NA MAJERAHA YA MOTO BAADA YA KUUNGUA USIKU WA KUAMKIA SEPTEMBA 13 MWAKA HUU.






















Kutokana na hali ya sintofaamu ambayo inaendelea kutanda katika kitongoji cha Nyabikondo kijiji cha Kewanja Kata kemambo Nyamongo Wilayani Tarime mkoani Mara baada ya matukio ya hivi karibuni ya kuungua moto Nyumba 11 na kupelekea hasara kubwa kwa wananchi bado suala la kuungua nyumba moto linaendelea ambapo kuamkia septemba 13 mwaka huu watoto wanne wamejeruhiwa kwa moto baada ya nyumba kuungua moto majira ya saa saba husiku
Aidha watoto hao walionusurika na moto ni Mwita Chacha wakiwemo watatu wa familia moja ambao ni ,Agustino Karuma,Wankuru Karuma pamoja na Benjamini Karuma ambapo baadhi yao wamelazwa katika Hospitali ya Nyangoto Nyamongo kwa ajili ya matibabu na hali zao zinaendelea vizuri
Hali hiyo ya kulipuka kwa moto bila kujua chanzo ni inazidi kuwaacha vinywa wazi na hofu ya maisha yao wakazi wa kitongoji cha Nyabikondo Kijiji kewanja Nyamongo Wilayani Tarime mkoani Mara ambapo wanazidi kuiomba serikali kuingilia kati mara moja  ili kubaini chanzo cha moto huo.
Kuruma  Zacharia  ni mkazi wa kitongoji cha Nyabikondo kijiji kewanja ambaye ni baba wa familia ya watoto watatu waliojeruhiwa kwa moto alisem akuwa baada ya matukio ya nyuma ya nyumba kuungua moto aliomba watoto wake kkujifadi kwa jirani ambapo nyumba ni ya bati kwani nyumba zilizokuwa zinaungua ni za nyasi lakini ameshanga usiku wa saa saba watoto wakipiga kelele kuwa moto unachoma nyumba kwa jirani nyumba ambayo ni ya bati.
Zacharia alisema kuwa baada ya kusikia kelele aliweza kukimbia na kuanza kuokoa watoto hao huku nyumba ikiwa imetanda moshi sehemu zote na kukimbiza bada majira ya saa nane usiku watoto hao katika Hospitali ya Nyangoto Nyamongo.
“Moto huu umezidi kutushangaza jamani sisi wana kitongoji tulidhani nyumba zinazoungua ni za  nyasi tu lakini hata za bati zimeweza kuungua na watoto wangu watatu wamejeruhiwa sana”  alisema Zacharia.
Baada ya matukio hayo ambayompaka sasa hayajapatiwa ufumbuzi Ofisi ya mbunge wa jimbo la Tarime Vijijini John Heche  kupitia katibu wake Mrimi Zabron ameweza  kuwatembelea wahanga wa matukio hayo na kutoa msaada wa goro tano pamoja na mchele kilo hamsini huku akitoa pole kwa niaba ya Mbunge huyo.
“Mbunge anaendelea na vikao Dodoma lakini nimefika kwa ajili ya kumwakilisha nawapa pole wahanga wa matukio haya ambayo yanazidi kushangaza jamii poleni sana baada ya wiki mbili mbunge mwenyewe atafika kwa ajili ya kuwapa pole” alisema Katibu wa Mbunge.
Kemenya Piter Mwera kwa niaba ya mgaganga mkuu katika Hospitali ya Nyanngoto anadhibitisha kupokelewa kwa watoto hao huku akisema kuwa mopaka sasa hali yao inaendelea vizuri
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Kewanja kata ya Kemambo ambapo matukio hayo yanzidi kutokea tangu Septemba saba mwaka huu Tanzania Omutima anadhibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akizidi kuwaomba wananchi kuendelea kuchukua taadhali.
Baada ya kutokea kwa matukio hayo ya kulipuka kwa moto na kuchoma nyumba hovyo mpaka sasa nyumba 12 tayari zimechimwa ambapo kaya saba zimeisha kumbwa na janga hilo huku watoto wanne wakijeruhiwa kwa moto jamba ambalo limekuwa taaruki katika kitogoji hicho suala ambalo limepelekea wananchi  kutoa vitu nje huku wakilala nje kwenye miti kwa kuhofia kuungua na moto nakudai kuwa nyumba zinazoungua ni za nyasi lakini tukio la mwisho ambalo limejeruhi watoto ilikuwa ni nyumba ya bati na hapa wanananchi wanazidi kutoa kilio kwa serikali akiwemo diwani wa kata ya Kibasuka Rucy Manyata kuwa nafasi ya viongozi wa dini ni kubwa katika suala hilo.
Hata hivyo kabla ya kuungua kwa nyumba ya kumi na mbili mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luga aliweza kufika eneo la tukio na kuongea na wanachi huku akisema kuwa endapo watabaini anayechoma moto huo afikishwe kwenye vyombo vya sheria na siyo kulipiza kisasi.

.
MWENYEKITI WA KITONGOJI CHA NYABIKONDA AKIONESHA MAENEO YALIKUMBAWA NA JANGA LA MOTO NYAMONGO
NYUMBA ILIYOUNGUA NA KUJERUHI WATOTO WANNE
 
KATIBU WA MBUNE MRIMI ZABRON AKISHUDIA MOJA YA NYUMBA ILIUNGUA KWA ,MOTO
Powered by Blogger.