Multichoice yafanya mapinduzi makubwa kupitia punguzo la bei za vifurushi

dsc_0081

Multichoice Tanzania imeamua kunufaisha wateja wake kwa kufanya mapinduzi makubwa kupitia punguzo la bei na kuongeza  chaneli 8  kupitia huduma yake ya DStv. Huduma hizo mpya za punguzo la bei zitaanza rasmi kufanya kazi kuanzia tarehe 1 Novemba, 2016. Vifurushi hivyo vya DStv ni DStv Premium, Compact Plus, Compact, Family na Access. Punguzo hizo za bei ni kama ifuatavyo:
DStv Premium inapokea punguzo la asili mia 16%, kuanzia Novemba 1, na bei itakuwa TZS 184 000. Pamoja na hayo, ongezeko la chaneli 8. DStv Compact Plus, inapokea punguzo la asili mia 17%, na bei yake itakuwa TZS 122,500. Wateja wataendelea kufaidi burudani ya hali ya juu ya vichekesho, tamthilia, sinema, michezo na vinginevyo.
dsc_0052Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald  Baraka Shelukindo akielezea namna ya ujio wa vipindi  vipya vya DSTV pamoja na maboresho yake.
dsc_0053Duphney  Mlimuka Karaze Afisa uhusiano wa Multchoice Tazania akifuatilia tukio hilo
dsc_0076Bi. Tike Mwakitwange Afisa Rasilimali watu wa Multichoice Tanzania akifuatilia tukio hilo
DSTV TZMeneja mauzo wa Multichoice Tanzania, Bw.Salum Salum akifafanua moja ya maswali katika mkutano huo
Chaneli hizo mpya zitakazorushwa ni Vuzu AMP, Lifetime, Discovery channel,Crime & Investigation, History channel and Africa Magic Showcase. DStv Compact Plus, imeongezewa chaneli za michezo zitakazoendeleza msisimko kwa wapenzi wa mpira wa miguu kupitia  vipindi vya UEFA Champions Leagues, European Football leagues na Europa league. Hizo mechi zote zinapatikana kwenye stesheni za SuperSport 6 (SS6) na SuperSport 4 (SS4).
Kwa wapenzi wa filamu za kiafrika, watafaidi kupitia Nollywood , wapenzi wa tamthilia zakilatino  wataburudishwa na telenovelas pamoja na filamu za Bollywood.  Bila kusahau sinema zitakazopatikana kupitia chaneli za ROK, Eva Plus na B4U Movies.
DStv Compact inapokea punguzo la asili mia 5%, na bei yake mpya ni TZS 82 250. Kifurushi hiki kina faida ya kurusha Premier League na La Liga tangia mwanzoni mwa mwaka huu. Pamoja na hayo, wateja wa DStv wataongezewa chaneli za ITV Choice (DStv chaneli 123), TCM (DStv chaneli 137) na SS4. Kuanzia Novemba na kuendelea, wateja wa Compact  watafaidishwa na chaneli za  ROK, Eva Plus na B4U Movies!
dsc_0059Mkutano huo ukiendelea
dsc_0065Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mkutano huo
dsc_0116Mkutano huo ukiendelea
Kifurushi cha DStv Family kimepokea punguzo la asili mia 16% na bei yake mpya ni TZS 42 900. Kifurushi hichi kinapokea ongezeko la chaneli 5, ambazo ni B4U Movies, Eva, Eva Plus, SS4 na FOX. Kifurushi cha DStv Bomba kitafaidisha wateja wake kwa ongezeko la chaneli 3, na punguzo la asili mia 15%, bei yake mpya ni TZS 19,950. Punguzo hili la bei kwa kifurushi hiki itaanzia tarehe 15 Novemba.
Katika mkutano huo, Mkurugenzi Ronald Baraka Shelukindo alisema yafuatayo: Nia yetu kuu katika kufanikisha punguzo hilo la bei ni kuweza kunufaisha wateja wetu ili kuwapa huduma bora zaidi na kuthamini mchango wao katika muendelezo wa kampuni yetu.  Multichoice tunayo furaha kubwa pia kuwaalika wateja wapya ili waweze kufaidi kupitia huduma zetu. Mapinduzi haya ya punguzo za bei ni mwamko mkubwa sana katika kufanikisha malengo yetu sio tu hapa nchini, lakini Afrika nzima.
dsc_0129Anne Kansiime Balozo wa DSTV Afrika Mashariki 
dsc_0145Wanahabari na ‘Staff’ wa DSTV wakiteta jambo
dsc_0146Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald  Baraka Shelukindo akielezea namna ya ujio wa vipindi  vipya vya DSTV pamoja na maboresho yake
dsc_0154Wanahabari wakipata ‘kujisevia’ msosi 
dsc_0157Mambo yaliendelea kupendeza na yakawa kama hivi.
dsc_0081Maafisa wa Multichoice Tanzania wakiendesha mkutano huo mbele ya wanahabari (Hawapo pichani) mapema leo Oktoba 18.2016.
Powered by Blogger.