RC YAHYA AWASILI KAGERA K UANZA MAJUKUMU YAKE.
Mkuu wa mkoa Kagera mpya Kanali Yahya Ramadhani Kido tayari amewasili mkoani humo kuanza majukumu yake ya kuwatumikia wananchi.
Kanali Kido baada ya kuwasili uwanja wa ndege Bukoba leo hii Tarehe 11 Februari amepokelewa na watumishi mbalimbali wa ofisi ya mkoa sambamba na viongozi wa manispaa ya Bukoba akiwemo mkuu wa wilaya Bukoba Mhe Erasto Sima pamoja na wakuu wa kamati za ulinzi na usalama.
Mkuu wa mkoa huyo aliteuliwa Tarehe 6 Februari 2026 na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan akipokea nafasi ya aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Mhe Fatma Mwassa

.jpeg)
