Makamu wa Rais akemea Mimba za utotoni, awavaa Maofisa Ardhi asema serikali itatatua changamoto ya Maji Tanzania pia awataka viongozi kusimamia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan
ameuagiza uongozi wa wilaya ya Serengeti na wa mkoa Mara kukamilisha
haraka awamu ya kwanza ya ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo ili kuondoa
adha ya wananchi kusafiri kwenda mikoa ya jirani ya Arusha na Mwanza
kwenda kupata huduma afya.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa agizo leo 6-June-2017 kwenye mkutano wa hadhara mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara mara baada ya kutembelea ujenzi wa hospitali hiyo ya wilaya na kuweka jiwe la msingi.
Makamu wa Rais amesema kutokana na wilaya ya Serengeti kupata wegeni wengi kutoka nje ya nchi ambao wanaenda kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo ni muhimu kwa viongozi wa wilaya na mkoa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo kukamilisha ujenzi huo haraka ili wananchi waweze kupata huduma za afya za uhakika katika wilaya yao.
Makamu wa Rais amesema kukamilika kwa ujenzi huo wa awamu ya kwanza kutaondoa taabu kubwa wanayopata wananchi wa wilaya ya Serengeti katika kupata huduma ya afya karibu na maeneo yao.
Katika kuunga mkono jitihada hizo za ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Serengeti, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni Tano na amewaahidi wananchi wa wilaya ya Serengeti kuwa atakikisha fedha kutoka Serikalini ambazo zinatakiwa kupelekwa wilayani humo zinapelekwa haraka ili kukamilisha ujenzi huo.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan pia amewataka wananchi kote nchini kuunga mkono jitihada za Serikali za kupambana na rushwa na ufisadi ili kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na manufaa kwa wananchi wote.
Amewaomba wananchi nchini wasirudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa bali waendelee kubaini watu wanaofanya vitendo hivyo ili Serikali iweze kuwachukulia hatua kali za kisheria .
Kuhusu tatizo la mimba mkoani Mara, Makamu wa Rais ameonyesha kuchukizwa na vitendo hivyo na kuomba vyombo vya dola na wananchi kwa ujumla kushirikiana katika kukomesha mimba za utotoni mkoani Mara.
Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa maelekezo yote anayoyatoa katika ziara yake yatafanyiwa kazi ipasavyo ili kuondoa kero na changamoto zinazowakabili wananchi.
Mkuu huyo wa mkoa wa Mara ameomba wananchi wa Mkoa wa Mara kuwepa pembeni tofauti zao za kisiasa bali washirikiane na Serikali katika utekelezaji wa miradi yao ya maendeleo.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan bado anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara ambapo hapo kesho atafanya ziara katika wilaya za Butiama na Musoma mkoani Mara.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa agizo leo 6-June-2017 kwenye mkutano wa hadhara mjini Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara mara baada ya kutembelea ujenzi wa hospitali hiyo ya wilaya na kuweka jiwe la msingi.
Makamu wa Rais amesema kutokana na wilaya ya Serengeti kupata wegeni wengi kutoka nje ya nchi ambao wanaenda kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo ni muhimu kwa viongozi wa wilaya na mkoa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo kukamilisha ujenzi huo haraka ili wananchi waweze kupata huduma za afya za uhakika katika wilaya yao.
Makamu wa Rais amesema kukamilika kwa ujenzi huo wa awamu ya kwanza kutaondoa taabu kubwa wanayopata wananchi wa wilaya ya Serengeti katika kupata huduma ya afya karibu na maeneo yao.
Katika kuunga mkono jitihada hizo za ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Serengeti, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni Tano na amewaahidi wananchi wa wilaya ya Serengeti kuwa atakikisha fedha kutoka Serikalini ambazo zinatakiwa kupelekwa wilayani humo zinapelekwa haraka ili kukamilisha ujenzi huo.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan pia amewataka wananchi kote nchini kuunga mkono jitihada za Serikali za kupambana na rushwa na ufisadi ili kuhakikisha miradi inayotekelezwa inakuwa na manufaa kwa wananchi wote.
Amewaomba wananchi nchini wasirudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa bali waendelee kubaini watu wanaofanya vitendo hivyo ili Serikali iweze kuwachukulia hatua kali za kisheria .
Kuhusu tatizo la mimba mkoani Mara, Makamu wa Rais ameonyesha kuchukizwa na vitendo hivyo na kuomba vyombo vya dola na wananchi kwa ujumla kushirikiana katika kukomesha mimba za utotoni mkoani Mara.
Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa maelekezo yote anayoyatoa katika ziara yake yatafanyiwa kazi ipasavyo ili kuondoa kero na changamoto zinazowakabili wananchi.
Mkuu huyo wa mkoa wa Mara ameomba wananchi wa Mkoa wa Mara kuwepa pembeni tofauti zao za kisiasa bali washirikiane na Serikali katika utekelezaji wa miradi yao ya maendeleo.
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan bado anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara ambapo hapo kesho atafanya ziara katika wilaya za Butiama na Musoma mkoani Mara.
Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurudin Babu akisoma taarifa kwa Makamu wa Rais |
| Makamu wa Rais akipanda Mti katika Hospitali ya Wilaya inayojengwa |
Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt Charles Mingwa akipanda Mti
![]() | ||
| Makamu wa Rais akiweka jiwe la Msingi katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara. |
Wakati hu huo Wananchi
walipiga kelele wakati Mkuu huyo wa wilaya akitoa taarifa ya wilaya kuhusu chakula kwa
Makamu wa Rais,wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea wilaya hiyo kusikiliza
kero,kuangalia miradi ya kimaendeleo na kutoa shukurani za kuwapa ushindi chama
tawa(ccm) kuongoza nchi katika viwanja vya Mbuzi mjini Mugumu.
Wananchi hao
walisikika wakisema kuwa hali ya chakula ni mbaya,hata kama serikali imetoa
chakula cha msaada,na kwamba walimtaka aombe kuongezewa chakula cha msaada
ambacho kitauzwa na serikali wenyewe badala ya kuwaruhusa wafanya biashara
kununua chakula hicho kwa bei nafuu na kukiuza kwa bei elekezi.
Mwananchi
mmoja mjasilia mali Robi Nyamuhanga alisema ni kweli serikali ilitoa chakula
cha msaada ambacho walinunua kwa bei ya Tsh. 700 kwa kilo moja kwa maeneo ya
mjini na vijijini kwa Tsh.750,lakini chakula hicho watu walinunua kwa siku tatu
tu.
Nyamuhanga
alisema baada ya siku tatu chakula kile kilichukuliwa na wafanyabiashara ambao
waliuza kwa bei elekezi kwa siku mbili,baada ya hapo walipandisha bei na kuuza
kwa Tsh. 21,000 kwa debe tofauti na serikali ilikuwa Tsh.14,000.
Awali Mkuu
wa wilaya Baabu alisema kuwa hali ya chakula wilayani humo ni ya kuridhisha
kufuatia kuwepo kwa mvua za kutosha na kwamba baada ya mda mfupi watavuna.
Baabu
alisema serikali ilitoa chakula cha msaada Tani 400 ambazo walizigawa kwa kuziuza
kwa bei nafuu,ambapo wananchi walifanikiwa kukinunua na kutunza akiba.
Mbunge wa
jimbo hilo Marwa Ryoba alisema wilaya ya Serengeti ni wilaya ya chakula ambayo
hulisha mkoa kwa kuzalisha chakula kingi,nakwamba hali ya upungufu wa chakula
kwa sasa imetokana na ukame kufuatia mvua kutonyesha kwa wakati msimu wa kilimo
mwaka jana na mwaka huu mwanzoni.
Hata hivyo
Ryoba alimpongeza mkuu wake wa wilaya kuwa hufanya kazi kwa ushirkiano na
wananchi wote sanjari mbunge bila kujali itikadi za kisiasa hali ambayo
inaifanya wilaya hiyo kuwa mstari wa mbele kimaendeleo mkoani Mara.
Makamu wa
Rais Samia Suluhu aliwataka wananchi kuacha kupiga kelele kuhusu hali ya ukame
kwani kunyesha mvua na kutonyesha ni mapenzi ya Mungu,hivyo hakuna kiongozi
aliyezuia mvua kunyesha,aliwataka kufanya kazi kwa bidii bila kukata tama.
“Hata kama
kuna njaa sio kwa kiasi hicho mlichopiga kelele,ila njiani nimeona mashamba
makubwa nina uhakika mtavuna hivi karibuni na tatizo la njaa litakwisha.
