WAFUGAJI WAITIKIA UPIGAJI CHAPA MIFUGO.

 Displaying chapa4.jpg
  Na mwandishi wa MAKALIBLOG, S             Mifugo ikipigwa chapa.
WAFUGAJI wilayani Maswa mkoani Simiyu wameitikia agizo la serikali la upigaji chapa na utambuzi wa mifugo yao hali itakayowaondolewa wizi wa mifugo na kupunguza migogoro baina yao na wakulima.
Aidha Wafugaji hao wamesema kuwa zoezi hilo litawapunguzia milipuko ya magonjwa kwa kuwa mifugo yao inatambulika kwa alama na idadi halisi huku wakiowaomba wataalamu wa mifugo kuwafikia mara kwa mara na kundeleza mahusiano waliyoyaanzisha.
Wakiongea wakati wa upigaji chapa mifugo katika kijiji cha Mwaliga, kata ya Shishiyu wilayani humo walisema kuwa wamekubali kwa hiari yao kupigiwa chapa mifugo yao ili kuepusha kuibiwa mifugo, pia kutambua idadi ya mifugo wao na wafugaji wenyewe kutambulika.
Medardi Msugwa mkazi wa kijiji hicho alisema kuwa baada ya kupewa elimu na kutambua umhimu wa mifugo kupigwa chapa, wafugaji wenyewe wanaleta mifugo yao kwa hiari huku wakija na gharaza za kupigiwa chapa shilingi mia tano kwa kila mfugo.
‘’gharama ya shilingi mia tano kwa kila mfugo ni kubwa kama una mifugo mingi…hatuna namna inabidi tutoe kulingana na mahitaji ya serikali ya kuwa kila mfugaji apigiwe chapa mifugo yake ili iweze kutambulika’’ alisema Kija Msugwa.
Afisa Mifugo wa Wilaya hiyo,Dk Efreim Lema alisema kuwa zoezi hilo lipo kwa mujibu wa sheria  na linalenga kudhibiti  magonjwa ya mifugo, kudhibiti wizi wa mifugo, kuboresha mazao ya mifugo kama nyama kwa  kuboresha soko  la mifugo ndani na nje ya nchi.
Lema alieleza kuwa kufanyika kwa zoezi hilo kutasababisha  kupatikana kwa masoko  maalumu kwa ajili ya kuuza  mifugo yao  kwa bei nzuri na hivyo kukuza uchumi wao na taifa kwa ujumla.
Aidha aliwataka wananchi na wafugaji kupuuza uvumi unaonezwa kuwa serikali inapiga chapa mifugo hiyo ili kuitaifisha na  pia wataanza kulipia kodi baada ya mifugo yao kutambuliwa.
Na kuongeza kuwa zoezi hilo halina nia ya kukwamisha shughuli zozote za kimaendeleo ama serikali kuchukua mifugo ya wafugaji kama inavyodaiwa na baadhi ya watu  bali ni kuhakikisha inamwekea mfugaji miundombinu ya kisasa ili aweze kufuga  kwa tija  kama nguzo moja wapo ya kuimarisha uchumi wake na Taifa kwa ujumla.
Wilaya ya Maswa ndiyo wilaya pekee iliyoanza kutklza zoezi hilo mkoani Simiyu  na inatarajia kupiga chapa ng’ombe wapatao 445,732 katika Kata zote 36 zenye vijiji 120 ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali la kufanya utambuzi, usajili na ufuatiliaji wa mifugo.
Hata hivyo Upigaji chapa huo ni agizo la kisheria kwa mujibu wa sheria Namba 12 ya mwaka 2010 ya Utambuzi na Usajili sambamba na utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa alilolitoa hivi karibuni la kutaka kila mfugaji nchi nzima asajiliwe na mifugo yake ipigwe chapa.
 Displaying chapa 2.jpg
                                                 Mifugo ikipigwa chapa

Displaying chapa.jpg .Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa Mhandisi,Ally Mubaraka akizindua zoezi la upigaji chapa kijiji cha Shishiyu wilayani Maswa.
 Displaying chapa 3.jpg
 .                                 Mifugo ikiandaliwa kupigwa chapa

Powered by Blogger.