WADAU WAKAHAWA WATOA MAAMZI YA PAMOJA KUBORESHA KAHAWA ILI KUKUZA SOKO LAO NDANI NANJE YA NCHI;
Na Mwandishi wa MAKALIBLOG; Mara.
Wadau wa kilimo cha kahawa kanda ya mara wameazimia Kwa pamoja kuboresha ubora wa kahawa yao ili kukuza soko LA bidhaa hiyo Katika soko la ndani na njee .
Wadau wa kilimo cha kahawa kanda ya mara wameazimia Kwa pamoja kuboresha ubora wa kahawa yao ili kukuza soko LA bidhaa hiyo Katika soko la ndani na njee .
Azimio hilo lilipitishwa Katika kikao cha pamoja kilicho
husisha wakulima , wataalamu wa kilimo na maafisa biashara pamoja na
viongozi Wa serikali kilicho fanyika Jana katika ukumbi Wa uwekezaji
uliopo katika ofisi za mkuu wa mkoa.
Naye afisa kilimo wa mkoa nyakisida Denis amesema kuwa ni
wakati sasa wa kutoa elimu kwa wakulima na vyama vya msingi kwa
kuwasaidia ili kuweza kuboresha mfumo utakao wezesha kutoa mapato ya zao
la kahawa kwa wakati muafaka.
Kwa upande wake Afisa biashara gambales timotheo
aliwaaasa viongozi wa vyama vya ushirika kuwa wawe wabunifu katika
kuboresha zao lao na kuweza kupata zao lenye ubora unao takiwa na wenye
tija.
Aidha kwa upande wake mkuu wa wilaya ya geita Herman kapufi
amesema kuwa atashirikiana vyema na wakulima ili waweze kupata miche
bora nakuwatafutia soko la uakika wakulima wa zao la kahawa wa wilaya
yake.