MKUU WA MKOA WA MARA KUZUNGUMZA NA WAKANDARASI;

 
mkuu wa mkoa wa mara akizungumza na wanahabari mara baada ya ukaguzi wa barabara ya makutano juu sanzate yenye km 50 hivi karibuni.

 
sehemu ya ujenzi wa barabara ya makutano juu sanzate ukiendelea;

Mkuu  wa mkoa wa Mara Daktari Charles Mlingwa  ameigaiza ofisi ya Meneja wa Tanrods mkoa wa Mara kuwaita wakandarasi wazalendo wote mkoani hapa kukutana kujadili utendaji wao.

Agizo hilo limekuja wakati mkuu wa mkoa wa Mara akifanya ukaguzi wa ujenzi na ukarabati wa barabara ya Mika Utegi Shirati kujengwa chini ya kiwango.

Mkuu wa mkoa huyo alisema lengo la kuwaita ni  kuwafahamisha jinsi serikali inavyotaka kazi inanywe baada ya kutoridhishwa na kasi ya ujenzi na ukarabati wa barabara ya lami nyepesi  ya Mika -Utegi  yenye urefu wa kilomita 8 inayogharimu sh 852 milioni.

“Na kuagiza uwaite haraka iwezekanavyo wakandarasi wote wanaohusika na ujenzi wa barabara zetu ili tuwafahamishe jinsi serikali inavyofanyakazi zake kwani kasi wanayoenda nayo haikidhi viwango tunavyotaka,” alisema Mlingwa.
Mlingwa alisema kuwa anataka kuwasikiliza wakandarasi wazawa ili kufahamu changamoto wanazokutana nazo jinsi wanayofanya kazi na kile serikali inavyotakiwa kufanyika na wafanye kwa kasi na kwa viwango vinavyotakiwa.
“Kikao hiki kifanyike mapema mwezi wa tano kazi ya utengenezaji wa kipande hiki hauniridhishi na uko chini sana ya kiwango, kwa sababu ni kweli tuwe na wakandarasi wazawa lakini pia kitumike kama sehemu ya kufahamiana, kwani

Kwa upande wake Meneja wa Tanroads mkoani Mara Mhandisi Mlima Felix aliwataka wananchi kutokujenga kando ya barabara ili badaye walipwe  na serikali (tegesha) ambapo watakuwa wanajidanganya na kupoteza muda wao ya kwamba watapata fidia.

“Tunachangamoto ya kukabiliana na wananchi kujenga kandokando na hifadhi ya barabara kwa lengo la kutegesha ili waje walipwe tunaomba serikali kuliangalia hili kwani limekwamisha ujenzi wa miradi ya barabara katika mkoa wa mara kukwama na kushindwa kukabidhiwa kwa wakati,”alisema Felix.


Powered by Blogger.