MIAKA 60 JELA KWA KOSA LA UNYANG'ANYI KWA KUTUMIA SILAHA



 

 Na   Eva-Sweet Musiba
MUSOMA- MARA
WATU wawili Jumanne Wambura(34) na Bkobe Bhoke(30) wakazi wa kijiji cha Pida Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara wamehumiwa kwenda jela kila mmoja miaka 30 kwa kosa la unyang’anyi kwa kutumia silaha
kinyume na kifungu cha sheria namba 287 A kanuni  ya adhabu iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002 na mapitio tena na sheria namba 3 ya mwaka 2011.



Akitoa hukumu hiyo, jana,hakimu mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Musoma,
Kharimu Mushi alisema kutokana  na ushahidi wa shahidi wa kwanza ambaye Mahakama ilimwona hana vidole  na wa pili, Mahakama hiyo imeona itoe adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa wengine na baada ya kifungo hicho watalipa Sh Milioni 2 kila mmoja kama sehemu ya malipo kwa majeraha aliyoyapata.


Alisema kuwa watu hao walitenda kosa hilo, septemba 29 mwaka 2014  na  baada ya kumkata kwa panga  vidole vitatu na kukatika walichukua Shilingi Milioni 1,200,000 mali ya Matiku Mwita.


Waendesha mashitaka walileta ushahidi wao, katika ushahidi, shahidi wa kwanza, Matiku Mwita(34) aliielezea Mahakama kuwa majira ya siku 6 za usiku katika eneo la Pida akiwa nyumbani kwake aliona watu sita aliwatambua hao ambapo mshitakiwa wa pili alivunja taa lakini tayari alikuwa amemwona  na kufanikiwa kuingia ndani na ndipo alipokatwa vidole vitatu vya mkono wa kushoto.


Aliendelea kwa kusema kuwa baada ya kumkata vidole vyake kwa maumivu makali aliyokuwa nayo alimwambia mkewe zilipo pesa ili atoe awapatie ili kunusuru roho yake,ambapo aliwatupia  fedha hizo kwa kuwatupia dirishani.


Naye shahidi wa pili Magreth Matiku aliiambia mahakama kuwa siku ya tukio aliona watu nje wakiwa na mapanga na marungu, walivunja mlango na kuingia ndani ambapo walimkata  kwa panga mumewe mkono wa kushoto na kuvuja damu nyingi na alitoa fedha ili kunusuru roho ya mumewe kwa kuzitupa nje kupitia dirishani na aliweza kuwatambua hao kwa kuwa nje kuna taa ya umeme wa jua (solar Power).


Naye mwendesha mashitaka, wakili wa serikali Frank Nchanila aliimbia Mahakama kuwa kwa kuzingatia kosa la unyang’anyi kwa kutumia silaha, vinaleta kifo na tayari Matiku Mwita ni mlemavu anaiomba Mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine.


Katika utetezi wao, mshitakiwa wa kwanza  aliiomba Mahakama kumpunguzia  adhabukwa kuwa amefanyiwa upasuaji ambapo wa pili alidai kuwa ana familia, mke na watoto sita na kwamba Mama yake Mzazi ni mlemavu  na ana  tatizo la bandama ambapo pia aliomba nakala ya hukumu.



Mashahidi wengine katika kesi hiyo walikuwa mpelelezi wa kesi hiyo,G 8299 PC Adam, Nyori Mwita na John Magesa.

MWISHO.
Powered by Blogger.