MSIBA MZITO MUSOMA VIJIJINI

 

TANZIA TANZIA TANZIA

Kijiji cha Nyasaungu kimeondokewa na Mdau Mkuu wa Maendeleo yao

Kwa masikitiko na majonzi mengi mno ninalazimika kutoa taarifa ya kifo cha mpendwa wetu Ndugu STEPHEN CHACHA MWITA WAMBURA (picha imeambatanishwa hapa)

Marehemu alipatwa na mauti kwenye ajali ya gari iliyotokea usiku wa Alhamisi (28 Nov) kuamikia Ijumaa (29 Nov) Jijini Mwanza!

Marehemu Chacha Mwita alikuwa Kiongozi wa jamii, Mchangiaji mkuu wa miradi ya maendeleo na Kada wa CCM.

Marehemu alichangia miradi yote muhimu ya Kijiji cha Nyasaungu:

1. Marehemu alikuwa mchangiaji mwanzilishi wa ujenzi wa S/M Nyasaungu

2. Marehemu alishirikiana na Mbunge wa Jimbo kwenye michango ya uboreshaji wa S/M Nyasaungu

3. Marehemu alikuwa mchangiaji mwanzilishi wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nyasaungu

4. Marehemu alishirikiana na Mbunge wa Jimbo kuendeleza ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nyasaungu


       Tunaishukuru Serikali yetu kwa kuchangia Tsh milioni 100 (Tsh 100m) kukamilisha ujenzi wa Zahanati hiyo itakayofunguliwa Januari 2025

5. Marehemu alishirikiana na Mbunge wa Jimbo kuanza kuchangia ujenzi wa Nyasaungu Sekondari ambayo imepangwa kufunguliwa Januari 2025


Poleni Wana-Nyasaungu tumempoteza mwenzetu tuliyeshirikiana nae kwa ukaribu sana kuchangia maendeleo na ustawi wa jamii yetu.

Kesho -Jumatatu, 2 Dec 2024* tutampuzisha mpendwa wetu mahali penye utulivu wa milele ulioko mikononi mwa Mwenyezi Mungu (Amen)

Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz

P. O. Box 6

Musoma


Tarehe:

Jumapili, 1 Dec 2024

 


 

Powered by Blogger.