TANESCO MKOANI MARA KUENDELEA KUPELEKA NEEMA VIJIJINI;
![]() |
| wafanya kazi wa shirika la umeme Tanzania TANESCO MKOANI MARA Wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho ya siku ya mazingira |
![]() |
| WAFNYA KAZI HAO MMOJA YA KAZI YAO KATIKA MAONYESHO WANAVYO FANYA KAZI |

Mmoja ya wataalamu wa TANESCO Akitoa maelezo kwa wananchi jinsi umeme unavyozalishwa, kusafirishwankusambazwa hadi kumfiki mteja ambayo ni hatua ya mwisho ya matumizi.
WANANCHI WAKIMFATILIA VIZURI MFANYA KAZI WA SHIRIKA HILO ALIVOKUWA AKITOA MAELEKEZO.
Shirika
la umeme Tanzania TANESCO Mkoani Mara limesema litashirikiana na
wananchi kuwapa huduma bora kutokana na kuendelea kuboresha huduma zao
kila kukicha.
Aliyasema
hayo Bwana Vesso ambae ni Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja mkoani
Mara na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano wa karibu kila wanapopata
matatizo katika maeneo yao, ambapo alisema
wakati umefika kwa wananchi kuacha kuharibu mazingira kwani TANESCO
wamejizatiti kundoa kero ya ukosefu wa umeme hapa nchini.
Pia aliongeza na kusema mpaka sasa upatikanaji wa umeme viijini mkoani Mara uko vizuri,vilevile gharama ya unit kwa wateja wa vijijini walio katika miradi ya REA ni nafuu kwani wanaweza
kupata unit 75 kwa gharama ya Tshs 9,150/- ambapo bei hii ya
kiwango cha chini inayoweza kumpa unafuu mtumiaji wa huduma ya umeme na
kuepukana na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti kwa ajili ya kuni na
matumizi mengine.
Aliongeza na kusema lengo la shirika ni kuwafikia watumiaji popote walipo.
Aliongeza na kusema lengo la shirika ni kuwafikia watumiaji popote walipo.
Aidha
amewataka wakazi wa mkoa wa Mara kuchangamkia fursa ya matumizi ya
kifaa cha UMETA unatumika kama mbadala ya udandazaji wa mifumo ya waya
ndani ya nyumba kwa wateja wenye chumba
kimoja hadi viwili.
Bwana Vesso aliongeza kwa kusema fursa hii yaweza kutumika kwa ajili ya kuendesha mitambo midogo midogo ya umeme wa njia moja zikiwemo salon,maduka ya vinywaji,kutengenezea juice n,k.
Bwana Vesso aliongeza kwa kusema fursa hii yaweza kutumika kwa ajili ya kuendesha mitambo midogo midogo ya umeme wa njia moja zikiwemo salon,maduka ya vinywaji,kutengenezea juice n,k.
Ujio
wa UMETA ni fursa bora kwa wananchi wa Tanzania na inaweza kusaidia
kuondoa tatizo la ajira katika maeneo yote ya nchini kwani kila mtu anao
uwezo wakutumia kifaa hicho kufungua biashara
ngodo na kujiajiri.
James Vesso amesema kuwa ataendelea kutoa elimu kwa wananchi ilikutumia neema kama hizi zinazojitokeza katika mkoa wa Mara.
Nami
mwandishi wa makaliblog nakamilisha kwa kusema Hongereni TANESCO lakini
jaribuni kwenda zaidi vijijini ambako lipo wimbi la vijana waliokosa
ajira lakini kwa kupitia umeme huu usiotumia
wayaring utawasidia kufungua ofisi zao na kujipata kipato na pengine
kusaidia familia zao kwa kujipatia mlo wa mara tatu kupitia mawazo yenu
mliyoaanzisha.
UNAWEZA KUTANGAZA NASI
TUPIGIE KWENYE
0754295996



