PROFESA MHONGO AWATAKA WANANCHI WAKE KUENDELEA NA SHUGHULI ZAO WALIZO ZIPANGA ZA MAENDELEO JIMBONI KWAKE;
![[IMG]](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6UkJbdYudiVPsXMH3103J8thmWQJTYBpu6xgv6iyhMnJw1XAOflKVtGM7GxtCMmINuyY9qUg02ARQC5hgTmaC4kMaZX8VFUUk8fvXnqIO8AtBiGj5VkWjhZl0xUJrlvkq2TS3jide_ak/s640/unnamed+%252816%2529.jpg)
NA Mwandishi wa MAKALIBLOG.MARA
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo amewataka wananchi wa Jimbo lake kuhakikisha wanaendelea na mipango yao ya shughuli zote za maendeleo ikiwa na ujenzi wa vyumba vya madarasa kama walivyokubaliana na kusahau yote yaliyotokea.
Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo amewataka wananchi wa Jimbo lake kuhakikisha wanaendelea na mipango yao ya shughuli zote za maendeleo ikiwa na ujenzi wa vyumba vya madarasa kama walivyokubaliana na kusahau yote yaliyotokea.
Akizungumza
na waandishi wa habari Katibu wa Mbunge Juma Ramadhani alisema kuwa wananchi wa
Jimbo hilo wanatakiwa kusahau yote yaliyotokea kwa mbunge wao na,kwamba kazi
iliyoko mbele yao ni ujenzi wa vyumba vya
madarasa pamoja na mipango mingine ya maendeleo waliyokuwa wamekwisha
ipanga katika jimbo lao.
“kazi
iliyoko mbele yetu ni ujenzi wa madarasa
na kadhalika,malengo yetu ni yaleyale na kasi ni ileile hakijaharibika
chochote,hivyo tujipange kwa ajili ya maendeleo ya Jimbo letu”alisema Katibu
huyo.
Ramadhani
alisema kuwa mbunge huyo pia amewataka
viongozi na wananchi wa jimbo hilo kujituma zaidi na kwa kasi zaidi katika
maeneo yao ndani ya vijiji na kata ili kuendelea na shughuli ujenzi wa Taifa.
Mmoja wananchi
wa Jimbo hilo nyasatu mafuru alisema kwa masikitiko kwa tukio la kutenguliwa kwa nafasi ya Uwaziri wa
Nishati na Madini mbunge wao,limewashitua sana lakini wanachofahamu ni kwamba
hata kama ameondolewa kwenye nafasi hiyo shughuli zao za maendeleo zitaendelea
kama kawaida na kama alivyokuwa amekwisha anza kutekeleza ahadi zake.
NA MAKALIBLOG MARA.
NA MAKALIBLOG MARA.