MAKAMU WA RAIS MHE; SAMIA SULUHU HASAN KUFANYA ZIARA MKOANI MARA SIKU YA MAZINGIRA;

 Image result for MAMA SAMIA KATIKA MIKUTANO MBALIMBALI
Na MAKALIBLOG. MARA
MKUU wa  Mkoa wa Mara Dk. Charles  Mlingwa amesema kuwa watatumia fursa ya
siku ya maadhimisho ya Mazingira  itakayofanyika katika wilaya ya
Butiama Mkoani humo   kuielimisha jamii  ili kuweza kukabiliana  na changamoto ya
uharibifu  wa mazingira
  hususani   uoto wa asili ambao umetoweka kwa
ajili ya wa kukata miti ovyo mkoa wa  Mara.

Ameyasema hayo wakati akitoa taarifa ya siku ya maadhimisho ya
mazingira Duniani ambayo  kitaifa  inafanyika katika Wilaya ya Butiama
waandishi kutoka vyombo mbalimbali   vya  habari   katika ukumbi wa
Uwekezaji uliopo ofisi ya Mkuu wa mkoa itakayofanyika katika wilaya ya
 Butiama Mkoani hapa.

Dk. Mlingwa alisema kuwa  maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa kuanzia
tarehe  1- 5 mwezi Juni kila  mwaka yatafunguliwa  na Juni 1  mwaka
huu katika viwanja vya Mwenge  Wilaya ya  Butiama ambapo  Makamu  wa
Rais  Samia suhulu Hassan atakuwa  Mgeni rasmi katika kilele cha
maadhimisho hayo na kufunguliwa Juni Mosi na Waziri wa Ncbi, Ofisi ya
Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira, January Makamba.

Aliongeza kuwa  maadhimisho hayo yatafuatana na kongamano
linalohusiana na masuala ya mazingira ikiwa ni pamoja  na upandaji wa
miche ya asili ipatayo 1,500 katika msitu wa Baba wa Taifa   ili
kuenzi  kazi zote  katika hifadhi ya mazingira .

  Alizitaja faida ambazo  mkoa huo utazipata kupitia fursa hiyo ya
maadhimisho kuwa ni pamoja  na  kuwajengea jamii uwezo juu ya uelewa
wa masula ya utunzaji wa  mazingira na changamoto za kijamii
zinazojitokeza katika utunzaji wa mazingira,kuwawezesha wadau
kushiriki katika fursa zinazohusiana  na upandaji  wa miti na kujadili
mwendelezo wa utekelezaji  wa shughuli zilizoratibiwa katika mkoa na
wizara kuhusu namna bora ya uhifadhi wa  mazingira.

Nyingine  ni   kuelimisha wananchi kupanda miti ili kukidhi mahitaji
ya  dunia kupambana   na ongezeko la hewa ya carbon Dioxide(ukaa)na
kuenzi kazi  zote za Baba wa  Taifa  Mwl. Nyerere katika utekelezaji
wa maendeleo hususani katika hifadhi ya  mazingira

                   
NA MAKALIBLO. MARA;

                 TUPE MAONI YAKO MATUSI HAPANA
Powered by Blogger.