AJIRA ZA MUDA TASAF ZAPUNGUZA ADHA YA MAJI ITILIMA.

Displaying IMG_20170524_130024.jpg
 Na Costantin mathias.SIMIYU.
Wanufaika wa ajira zamuda toka TASAF III wakiaonyesha moja ya visima walivyochimba kwa nguvu zao.

Wananchi Wilayani Itilima mkoani Simiyu wameanza kunufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF III) kupitia ajira za muda ambapo wameweza kuibua miradi ya kujiletea maendeleo kwa kujenga visima vya maji na Mabwawa.

Aidha ajira hizo za muda zilikuwa zikiwanufaisha walengwa wa TASAF kwa kulipwa ujira pindi wanapofanyakazi katika miradi hiyo waliyoiibua wenyewe kama kipaumbele katika maeneo yao.

Hayo yalibainishwa na Mhandisi wa maji wa Wilaya hiyo  Godluck Masige, mbele wadau wa maendeleo wanaofadhili mpango huo waliofika wilayani humo kukagua utekelezaji wa ajira za muda kwa wanufaika hao.

 “ wananchi waliibua vipaumbele vyao na Mpango ulikuwa ukitoa fedha kwa ajili ya kuvitengeneza visima hivyo ili viwe bora zaidi na salama, walioshirikia kuchimba walilipwa kupitia mpango ambao pia walikuwa ni walengwa, sasa hivi visima vyote vinatoa maji” alisema Masige.
Masige aliongeza kuwa Serikali Wilayani humo imeweka mpango wa kuviwekea pampu visima vyote 194 vilivyochimbwa kupitia mradi wa TASAF ili kuwarahisishia wananchi kupata maji kwa urahisi zaidi kuliko teknojia inayotumika sasa ya kuvuta maji kwa kamba.
 Alisema kuwa mbali na visima hivyo vijiji vingine wamechimba mabwawa ambayo yameanza kutumika na wananchi wenyewe ndiyo waliopewa fursa ya kuchagua mradi kama kipaumbele kikuu kwao.
Wanufaika wa TASAF III wameshukuru kwa kutatuliwa changamoto ya upungufu wa maji kwa mpango huo kwa kutoa ajira za muda katika uchimbaji wa visima vya maji na kuomba kuongezewa idadi ya visima hivyo katika awamu nyingine ya utekelezaji wa mradi ili waweze kuondokana na adha ya ukosefu wa maji
“Tunaishukuru sana TASAF kutuletea maji kwa visima hivi kupitia ajira za muda, tulikuwa tunatembea muda mrefu sana zaidi ya saa moja kufuata maji, lakini sasa hivi maji yapo karibu tena ni maji safi na salama” amesema Lubili Noni mkazi  wa Migato.
Kilolo Magige na Mahila Limbu ni wananchi walionufaika na miradi hiyo, wanaeleza kuwa wamekuwa wakihangaika kutafuta maji ambapo mpango huo umewawezesha kuondokana na changamoto hiyo.
Kwa upande wake Dampo Ndenzako kutoka shirika la kazi Duniani, ajira za muda na hifadhi ya jamii, alishauri serikali kuendeleza miradi ambayo inatekelezwa na TASAF hasa inayoibuliwa na wananchi kupitia ajira za muda.
Alisema kuwa kuwepo kwa mabwawa yatasaidia kuongeza fursa ya kilimo kwa wananchi kwa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji na kupata fedha za ziada.

‘’mipango ya TASAF lazima pawepo na ushirikiano toka ngazi za serikali na wataalamu  ili waweze kuwatembelea wananchi hawa pindi wanapoibua miradi ili iwez kuwa endelevu’’ alisema Ndenzako.
Wilaya Itilima ni moja ya Wilaya tano zinazofanyiwa tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini (TASAF III) katika awamu hii, tathmini inayofanywa na wataalam kutoka TASAF Makao Makuu, Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo (wadau washiriki wa mradi) ambao ni UNDP, UNFPA, ILO pamoja na Umoja wa Nchi za Ulaya(EU).

Displaying Maji Migato.jpgWanufaika wa TASAF III kutoka kijiji cha Migato wilaya ya Itilima wakichota maji katika moja ya visima vilivyochimbwa na TASAF kupitia programu ya kazi za ajira za muda katika kijiji hicho.
Displaying Maji 2 Migato.jpg

Displaying IMG_20170524_130050.jpg
 Kibao cha Mradi wa Maji cha TASAF.
NA. MAKALIBLOG.
Powered by Blogger.