SAFARI YA KUMUUNGA MKONO RAIS KUHUSU VIWANDA MARA YATANGULIA MWEKEZAJI MoU ASAIN KUJENGA KIWANDA CHA SUKARI




 Uchumi wa viwanda: Safari ya kuanzisha viwanda katika Wilaya ya Tarime imeanza rasmi leo baada ya kampuni ya Nile Agro Industries Limited ya Uganda kusaini Makubaliano(MoU) ya kujenga kiwanda  cha sukari Wilayani Tarime.


Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika leo katika ukumbi wa uwekezaji  katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na kushuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa, viongozi wa jamii kutoka vijiji vinavyotegemea kunufaika na uwekezaji huo, wafanyabiashara wakiwemo wakandarasi wa Wilaya ya Tarime.
Akitaja faida za uwekezaji huo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga amesema ujenzi wa kiwanda hicho utatoa ajira (direct employment) 5,000, na indirect employment kwa watu  10,000  pamoja na kusadia wakulima kuanzisha kilimo cha miwa kama zao lao la biashara.
DC Luoga uwekezaji huo utaiwezesha pia Halmashauri ya Wilaya ya  Tarime kuongeza mapato yake  kupitia ushuru wa huduma na kodi zingine zitakazokuwa zikilipewa serikari kuu.
“ Uwekezaji huu utabadilisha Tarime na Mara  kilimo cha miwa itakuwa dhahabu isiyoisha”, amesema Luoga  na kuongeza kuwa tayari kuna eneo lenye ukubwa wa hekta 4439 ambalo liko tayari kwa ajili ya uwekezaji huo na hekta zingine 1,297 kwa ajili ya wakulima wadogowadogo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara  Dkt Mlingwa amemkaribisha mwekezaji huyo na kumuahidi ushirikiano wa kutosha.
Dkt Mlingwa amempongeza pia Mkuu wa Wilaya ya Tarime kwa juhudi ambazo amefanya kuanzishaji wa kilimo cha miwa na kiwanda cha sukari.
“ Kwa namna ya pekee kabisa nakupongeza Mkuu wa Wilaya ya Tarime (Luoga)  na timu yako kwa kufikia hatua hii”, amesema RC Mlingwa.
Akiongea baada ya kusaini makubaliano hayo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Tarime Moses Misiwa amesema ujio wa mwekezaji huyo ni neema kubwa kwa wanatarime na kusema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha uwekezaji huo unakuwa na mfanikio makubwa.
Mwenyekiti wa Nile Agro Industruries Limited Patel Magan na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Patel  Gajendra wameshiriki kusaini makubaliano hayo na kusema wako tayari kujenga kiwanda hicho bila kuchelewa.

Viongozi wa Halmashuri ya Wilaya Tarime na kampuni ya Nile Agro Industries wakisaini makubalion ya ujenzi wa kiwanda cha sukari Tarime. Katikati (mstari wa nyuma) ni Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt Charles Mlingwa akishuhudia tukio hilo

 


RC Mlingwa akizungumza katika hafla hiyo


Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga akitaja faida zitakazotokana na uwekezaji wa  kiwanda cha sukari

Picha ya pamoja baada makubaliano ya kujenga kiwanda cha sukari katika Wilaya ya  Tarime

Powered by Blogger.