HARUSI ISIYO NA GHARAMA YAZUA GUMZO..WAMETUMIA SHILINGI ELFU 2 TU..SHUHUDIA
Wanandoa wawili ambao taarifa yao ya 
harusi isiyo na gharama imezua gumzo na imevutia watu wengi katika 
mitandao ya kijamii na sasa watagharamiwa honeymoon (fungate) ya harusi 
hiyo.
Wilson mwenye umri wa miaka 26 na Ann 
Wambui mwenye umri wa miaka 24 alitumia shilingi za Kenya 100 sawa na 
shilingi 2,147 ya Tanzania,kununua pete mbili mbali na kuvaa tisheti za 
sherehe hiyo.
Hawakuwa na sherehe yoyote baadaye.
''Tulienda nyumbani, tukapika ugali na 
sukuma wiki tukala na kulala,hapakuwa na kitu chochote maalum ambapo 
tungefanya kama fungate yetu'', kulingana na eDaily News.
Kiongozi wa dini ambaye alihalalisha 
ndoa hiyo alisambaza habari yao katika mtandao wa facebook kabla ya 
kuchukuliwa na vyombo vya habari.
Mwakilishi wa kampuni ya Bonfire Adventure alikutana na wanandoa hao.

Wilson na Ann Wambui wakifunga ndoa
Wilson na Ann Wambui

 


 
 
 
 
 
