Waziri Ummy atoa siku 60 wakurugenzi kuwapa wauguzi pesa za sare

Wakurugenzi
 wa halmashauri na wale wa hospitali za umma nchini wamepewa siku sitini
 kuanzia jana wawe wamewalipa posho za wauguzi za kununua sare za kazi 
ya shilingi laki moja na elfu ishirini pamoja na malimbikizo ya sare 
hizo.
Agizo
 hilo limetolewa mkoani hapa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia
 ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa 44 
wa wauguzi Tanzania.
Waziri
 Ummy alisema asilimia themanini ya kazi zote kwenye sekta ya afya 
nchini zinafanywa na wauguzi,hivyo aliwataka wakurugenzi kuzingatia 
miongozo iliyopo ya Serikali, “kama mwongozo ni kulipa elfu thelatini 
lipa thelathini si vinginevyo. Serikali imekwishatoa waraka wa kazi za 
ziada yaani “extra duty circular” ambao unapaswa kufuatwa hata 
mnapofanya kazi usiku kwani kuna masaa ya ziada”.
“Nawaagiza
 waajiri wote kuzingatia nyaraka hizi ili kuondoa malalamiko yasiyo ya 
lazima, Hili ni suala muhimu kwani mnakuwa kazini siku tano hadi sita 
kwa wiki hivyo mnahitaji sare walau tano ili muweze kubadilisha kila 
mara. Serikali itatoa waraka wa si chini ya laki tatu kulingana na hali 
ya uchumi itavyokuwa. Natumaini waraka huu utatoka mapema na kuanza 
kutumika mwaka ujao wa fedha hivyo kwa mwaka huu tuendelee kutumia 
waraka uliopo.
Aidha,
 aliagiza baada ya siku sitini alizotoa kupatiwa orodha za halmashauri 
ambazo hazitokuwa zimewalipa posho hizo na mikoa ipi”kwani kuna wauguzi 
wangapi hadi mshindwe kuwapa posho za sare ,mnataka wauguzi hawa waje 
kazini wawe wamevaa nini?aliuliza Waziri
Akijibu
 tatizo la kusimamishwa na kufukuzwa kazi kwa wauguzi na wakunga alisema
 ,suala la kusimamisha au kumwachisha kazi mtumishi lina taratibu zake 
ambazo zinapaswa kufuatwa.
“Napenda
 kuliagiza Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania kuwaelimisha waajiri 
kuhusu hatua za kufuata katika kushughulikia malalamiko yanayotolewa na 
wananchi ili yaweze kusikilizwa kwa utaratibu zilizopo bila ya kuwaonea 
pande zote, Ni kweli kuwa unapoadhibiwa bila kosa inavunja moyo, Naomba 
ieleweke kuwa sio nia ya Serikali kuwaumiza wauguzi bali lengo letu 
kubwa ni kuondoa kero za wananchi ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia 
watumishi wote wazembe na wasiofuata maadili ya kazi”.
Hatahivyo
 Waziri huyo ametoa rai kwa jamii kuweza kuwaheshimu wauguzi na wakunga 
kwani kumtukana na kumnyanyasa ni kutomtendea haki kwani wauguzi 
wanatakiwa kupendwa na kuthaminiwa”wahenga walisema usitukane mkunga na 
uzazi ungalipo,hivyo wananchi msiwatukane wauguzi kwani mkeo au mtoto 
wako atajifungua na atasaidiwa na huyo mkunga,tuwapende na kuwaheshimu 
wauguzi”.
Aliwataka
 Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuweka namba maalumu za wananchi kutoa
 malalamiko na kwa upande wa viongozi kuondoa urasimu wa kushughulikia 
malalamiko hayo kwa kuweka utaratibu mzuri wa kuwashughulikia ambayo 
yamezidi na yanakatisha tamaa kwa kada hiyo.
Kuhusu
 upungufu mkubwa wa wauguzi Waziri Ummy alisema ni kweli kuwa, nchi 
inakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa wauguzi hali inayopelekea 
muuguzi mmoja kuhudumia wagonjwa wengi zaidi ya uwezo wake,Mazingira 
hayo yanaweza kuathiri ubora wa huduma wanayotoa.
“Serikali
 inaendelea na jitihada za kuhakikisha watumishi wa afya wenye weledi wa
 kutosha wakiwamo wauguzi wanapatikana na kupangiwa katika vituo vya 
kazi sehemu mbalimbali za nchi yetu, Napenda nitumie fursa hii 
kuwahakikishia kuwa Serikali imepanga kuongeza idadi ya wauguzi nchini 
kila mwaka mara tu zoezi la kuwaondoa watumishi hewa kukamilika 
ninaamini Sekta ya Afya itapewa kipaumbele cha kwanza katika ajira mpya.
 Hivyo, niwaombe muendelee kuwa wavumilivu na kutoa huduma vema kwa 
kuzingatia taaluma yenu wakati jitihada za kuongeza watumishi 
zikiendelea”.
Wauguzi
 nchini wamekuwa na utaratibu wa kukutana kitaifa na kuelimishana juu ya
 maadili,majukumu ya viongozi wa chama katika utoaji wa huduma za afya 
kwa weledi kwa magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza.Mkutano 
umebeba ujumbe maalumu na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Wauguzi :nguvu ya 
mabadiliko,uboreshaji wa uthabiti wa mfumo wa afya.