Serikali kuanza kutoa chanjo ya kujikinga na saratani

Baada ya idadi ya wagonjwa wapya wa saratani kuongezeka kila siku hasa katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.
Serikali imeanza kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kuzuia na Kudhibiti Saratani kwa kuongeza juhudi za upimaji wa dalili za saratani pamoja na kutoa chanjo dhidi ya kirusi cha HPV kwa wasichana, ili kuondokana na tatizo hilo.

Baada ya idadi ya wagonjwa wapya wa saratani kuongezeka kila siku hasa katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.
Serikali imeanza kutekeleza Mkakati wa Kitaifa wa Kuzuia na Kudhibiti Saratani kwa kuongeza juhudi za upimaji wa dalili za saratani pamoja na kutoa chanjo dhidi ya kirusi cha HPV kwa wasichana, ili kuondokana na tatizo hilo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Julius Mwaiselage na wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Matembezi ya Hisani ya Kuhamasisha Uchunguzi na Kuchangia Matibabu ya Saratani ya Matiti.
Amesema takwimu zinazotolewa na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinaonyesha kuwa wagonjwa wapya milioni 14.1 hugunduliwa kila mwaka duniani.
Na kwamba kati ya wagonjwa hao, milioni 8.2 hufariki dunia kila mwaka. Hata hivyo amesema vifo vitokanavyo na saratani vinategemewa kuongezeka na kufikia milioni 22 ifikapo mwaka 2030.
Mwaiselage amesema hapa nchini, idadi ya wagonjwa wapya kila mwaka ni 44,000 na kwamba idadi hiyo ni sawa na asilimia 12.5 ya wagonjwa wanaofika katika Taasisi ya Ocean Road kwa ajili ya uchunguzi wa kitaalamu na matibabu.
Amesema, asilimia 80 ya wagonjwa hao hufika hospitali wakiwa katika hatua za juu za ugonjwa hali ambayo hupunguza uwezekano wa kupatiwa matibabu ya kuponyesha ugonjwa.
Mwaiselage amesema Taasisi hiyo hadi sasa imehudumia wagonjwa wa saratani 33,563 wakiwemo wagonjwa wapya na wale wa marudio 20,297.
Pia taasisi hiyo ilifanya uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya uzazi kwa watu 7,134 ambapo watu 570 walikutwa na dalili za awali za saratani.
Kuhusu matembezi hayo ya hisani yanayotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2016, Mwaiselage amesema lengo la matembezi hayo ni kuchangia juhudi za serikali katika kutokomeza saratani ya matiti, kuchangia ununuzi wa vifaa vya kutolea tiba pamoja na kuendesha zoezi la uchunguzi wa saratani hiyo
Powered by Blogger.