WANA CCM SERENGETI WATOA YA MOYONI


 
MWENYEKITI wa  Kijiji cha Nyamburi,kata ya Sedeko tawi la Bisarara Wilaya ya Serengeti Mkoa wa Mara,Samsoni Matiku amekiomba Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara kutoa kadi za Chama kwa wanachama ili kuepuka matatizo mbalimbali yaliyotokea katika Uchaguzi wa mwaka Mkuu wa mwaka 2016 na kusababisha kupoteza jimbo.

Akizungumza katika kikao chao kilichoitishwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Innocent Nanzabar cha makatibu  wa Chama  cha Mapinduzi ( CCM) wa matawi na Jumuiya zake  pamoja na Sekretaireti  katika wilaya hiyo alisema kuwa kutotolewa kwa kadi za uanachama kulisabibisha kupoteza jimbo la Serengeti jambo ambalo liliwazunisha kwa kupoteza aliyekuwa Waziri wa Afya,Steven Kebwe ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyekuwa msaada kwao.

Aidha ametoa shukrani kwa viongozi wa Chama kuwafikia kwani walikuwa wamesahaulika na kwamba walikuwa wamesahau majukumu yao ya kuwahadhibu wanachama ambao walikuwa wanakiuka kanuni za Chama kwa uzembe na kukiuka maadili na kusababisha Chama kuwa na makundi ya ukabila.

Naye Mwenyekiti wa Serikali wa Kijiji hicho, Mgendi Mniko ambaye alishuhudia kuzaliwa kwa CCM mwaka 1977  mjini Dodoma alisema kuwa vijana wa sasa hawatambui historia ya Chama kutokana na kutopewa katiba na Ilani ambayo enzi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere ilikuwa kama biblia ama Msaafu  na kuomba uongozi wa Chama kugawa Ilani na katiba ya Chama ili wanachama waweze kuisoma na kuielewa.

Akijibu hoja zao, Katibu wa CCM Mkoa wa Mara, Innocent Nanzabar alisema kuwa kwa sasa Chama kimetambua masuala yaliyokuwa yanasabisha wananchama wake kutojitokeza kutokana na kuwasahau mabalozi ambao ndo walikuwa wenye Chama na kwamba Chama kimerudishwa kwa wenye Chama.

Aliwataka kuwa makini katika utekelezaji wa majukumu ya kazi  zao ili  kuweza kupata takwimu  za wanachama zilizo sahihi  kuanzia ngazi ya mashina  na Matawi na kuhakikisha wanalipa ada za Chama.

Akizungumza katika  kikao kilichofanyika katika ofisi ya kata ya Mbalibali aliwataka mabalozi hao kuchukua fomu za kugombea nyadhifa za juu na kufanya na kuhakikisha   zoezi la uchukuaji wa fomu ngazi ya kata kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa mwaka 2019 /2020 linafanywa vizuri bila kificho.

Nanzabar  alisema kuwa lengo la ziara yake katika Mkoa wa Mara kati ya matawi 180 yaliyopo  ametembelea  kata 80  kwa nia ya kuimarisha chama na kuwatambua viongozi wa matawi waliochaguliwa katika uchaguzi uliomalizika hivi karibuni na  mabalozi na kutoa elimu juuu ya muundo mpya wa uongozi uliofanyiwa marekebisho.
Powered by Blogger.